Wito wa kuchukuliwa hatua za kijeshi dhidi ya Iran umeibuka tena huku kukiwa na mvutano wa kieneo, lakini tajiriba ya kihistoria inaonyesha kuwa mkakati kama huo hauwezi kuwa na mafanikio.
Katika toleo la hivi majuzi lililopewa jina la "Trump Hapaswi Kurudia Kosa la Saddam: Usishambulie Iran," gazeti la The Hill linasisitiza kwamba Iran sio nchi inayokaribia kuporomoka, kama baadhi ya watu wenye msimamo mkali wanavyodhani. Badala yake, ni taifa imara lenye uwezo wa kuungana dhidi ya vitisho vya kigeni. Sehemu ya makala hiyo inaitaka Marekani kuikaribia Iran kwa uelewa wa kweli wa mshikamano wake na kujitolea kufanya mazungumzo badala ya uchokozi.
Makala hiyo inalinganisha kati ya hali ya sasa na Vita vya Iraq na Iran vya 1980, wakati dikteta Saddam Hussein alipoihukumu vibaya Iran ya baada ya mapinduzi kuwa dhaifu na iliyogawanyika. Kinyume na dhana hiyo, Wairani waliungana katika misingi ya kitaifa na kisiasa kutetea nchi yao, na kugeuza kile ambacho Saddam alitarajia kuwa mzozo mfupi kuwa vita vya miaka minane na vifo vingi.
Gazeti la The Hill linaonya kwamba Marekani ina hatari ya kurudia kosa la Saddam Hussein la 1980 la kudharau uwezo na uwiano wa ndani wa Iran baada ya mapinduzi, ambayo ilisababisha vita vya muda mrefu na vya gharama kubwa badala ya kuanguka kwa utawala wa haraka. Mwandishi anamalizia makala yake kwa kumtaka Rais wa sasa wa Marekani Donald Trump asirudie kosa la Saddam.
342/
Your Comment